SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi na Mjumbe wa kamati kuu ya CCM taifa Komred Kheri James leo ameendelea na Ziara yake ya kikazi ya kuimarisha Uhai wa Chama na Jumuiya katika wilaya ya Iringa Vijijini Mkoa Iringa.

Akiwa wilayani humo komred Kheri James amezungumza na Mabaraza yote ya Jumuiya za CCM wilayani humo Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Siasa Na kilimo.

Akizungumza na wajumbe wa Mabaraza hayo Komred kheri James amewasihi kuendelea kisimamia Serikali katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ili kuleta maendeleo na ustawi wa wananchi kama tulivyowaahidi katika uchaguzi Mkuu uliopita.

Aidha Komred Kheri James ametoa pongezi za dhati kwa Halimashauri ya iringa Vijijini kwa kutekeleza kwa vitendo zoezi la uwezesheji wa vijana kiuchumi jambo ambalo limechochea vijana kuwa wabunifu na kujiajiri katika shughuli mbali mbali za uzalishaji mali.

Akikamilisha ziara yake wilayani iringa Vijijini komred kheri James allipata fursa ya kutembelea Shamba la Umoja wa Vijana Igumbilo na kuona utekelezaji wa kilimo cha kisasa Cha Mahindi,Maharage na Alizeti.Akiwa shambani hapo komred kheri james amewashukuru na Kuwapongeza vijana wote kwa kuendelea kusimamia vyema shughuli za kilimo katika shamba hilo ambalo linatumika kwa uzalishaji wa Chakula kinachotumiwa na Chuo cha Umoja wa Vijana ihemi pamoja na biashara kwa ajili ya uwendeshaji wa Shughuli za Chuo ,Na amesisitiza kuwa Umoja wa Vijana utaendelea kuwa ni jumuiya ya mfano katika kufanya shughuli za uzalishaji mali kama shamba darasa kwa vijana wengine kujifunza.

Katika ziara hiyo komred kheri James ameongozana na Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Brown mwangomango,katibu Wa Idara ya Uchumi na Fedha UVCCM Ndg Nelson lusekelo pamoja na wajumbe wa kamati ya utekelezaji Mkoa wa Iringa

Kesho komred kheri James ataendelea na Ziara yake ya kuimarisha Uhai wa chama Na Jumuiya katika wilaya ya Iringa Mjini.




Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020