Posts

Showing posts from September, 2020

ASANTE SANA IRINGAAAA! ASANTENI KWA KUJA SAMORA!

Image
  Maelfu ya watu waliojitokeza katika uwanja wa Samora mjini Iringa wakati wa ziara ya Mgombea URAIS kwa tiketi ya CCM, Rais John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM  Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iringa mjini akiwa na mtoto uwanja wa Samoraaa

DK NYAMAHANGA AMUHAKIKISHIA RAIS MAGUFULI USHINDI WA KISHINDO IRINGA

Image
  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Dk Nyamahanga amemuhakikishia Rais John Pombe Magufuli ushindi wa kishindo kwa madiwani wote, wabunge na Rais. Dk Nyamahanga alizungumza wakati akimkaribisha Rais John Pombe Magufuli, kuzungumza na maelfu ya wakazi wa Iringa waliokuwa wamefurika katika mkutano wa kampeni, kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa.

Pinda; Wabunge wa Iringa watashinda, CCM tumejipanga vizuri sana!

Image
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mlezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Peter Pinda amesema wagombea ubunge wote wa CCM katika mkoa huo, likiwemo Jimbo la Iringa mjini watashinda. "Tumejipanga vizuri sana ndio maana hata katika kuhamasisha watu kuja uwanjani kazi imekuwa nyepesi sana," amesema. Pinda alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa Mgombea Urais, John Pombe Magufuli uliofanyiwa uwanja wa Samora ambao mamia na wananchi wa Iringa walihudhuria.

"ZAMU YETU IRINGA IMEFIKA, KARIBUNI WANANCHI WOTE," - DKT ABEL NYAMAHANGA, MWENYEKITI WA CCM MKOA WA IRINGA

Image
 "Karibuni sana uwanja wa Samora, tusikilize sera za Mgombea wetu, Rais John Pombe Magufuli ili Octoba 28, tusifanye kosa," Dkt Abel Nyamahanga, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa.

"KARIBUNI IRINGA, KARIBU USIKILIZE SERA ZA CCM, SERA ZA MGOMBEA WETU, RAIS JOHN MAGUFULI" - MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA

Image
    "Wananchi wote wa mkoa wa Iringa naombeni mjitokeze kwa wingi kwenye mkutano wa Mh Dk John Pombe Magufuli, Mwenyekiti wa CCM Taifa na Mgombe wa URAIS kupitia CCM. Ni uwanja wa Samora," Salim Asas - Mnec

Bilioni 179.371 zatumika kutengeneza Barabara - Utekelezaji wa Ilani ya (CCM 2015-2020)

Image
  UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM 2015-2020 #MKOA_WA_IRINGA_BARABARA Serikali kupitia Wakala wa Barabara imetoa jumla ya Shilingi 179.371 Bilioni kwa ajili ya kutengeneza barabara zenye urefu wa kilomita 6,146.14 na madaraja 760 kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2015 mpaka 2020 #JPM ✓

Kihenzile aahidi ujenzi wa kituo cha Afya Idete - Mufindi Kusini

Image
  "Kuna umuhimu mkubwa wa hapa Kidete kuwepo kituo Cha afya, hapa naombeni miaka mitano tu nilisimamie hili, ili tuweze kuokoa ndugu zetu wanaopoteza Maisha kwa kukosa huduma ya afya, hasa akina mama, watoto na wazee. David Kihenzile Mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Mufindi kusini.

Mikopo iliyotolewa kwa wanawake na vijana yafikia Sh712.4 Milioni - Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2015-2016 (Iringa)

Image
  Utekelezaji Ilani ya CCM 2015-2020 Mkoa wa Iringa Mikopo iliyotolewa kwa wanawake na vijana katika mkoa wa Iringa imeongezeka kutoka Sh183.6 Milioni hadi kufikia Sh 712.4 Milioni 2019/2020.   Tumetekeleza kwa Kishindo, Tunasonga mbele Pamoja  

UPATIKANAJI WA MAJI SAFI NA SALAMA WAFIKIA ASILIMIA 74.2 TOKA ASILIMIA 69.3 mwaka 2015 - Ilani ya CCM (2015-2020 MKOANI IRINGA)

Image
Utekelezaji wa Ilani ya CCM - Mkoa wa Iringa (2015-2020) Hali ya upatikanaji wa maji safi na salama mkoani Iringa imeongezeka kutoka asilimia 69.3 mwaka 2015 mpaka kufikia asilimia 74.2 mwaka 2020. Idadi ya wanaopata huduma ya maji ni 812,612 kati ya watu 1,095,172.  Tumetekeleza kwa Kishindo, Tunasonga Mbele Pamoja

123,154 WAFIKISHIWA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA VIJIJINI - UTEKELEZAJI ILANI YA CCM 2015-2020 (IRINGA)

Image
  Utekelezaji Ilani ya CCM - Mkoa wa Iringa (2015-2020) Zaidi ya wananchi 123,154 wamefikishiwa huduma ya maji safi na salama kupitia Program ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa kuvifikia vijiji 43 vya mkoa wa Iringa katika kipindi cha mwaka 2015-2020 kwa gharama ya Sh20.3 Bilioni. Pia miradi 29 ya maji itakayogharimu Sh22.938 Bilioni inaendelea kutekelezwa kwenye vijiji 71 vya mkoa wa Iringa na kutarajia kuwafikia wananchi zaidi ya 239,395 Tumetekelezakwa Kishindo, Tunasonga Mbele Pamoja  

BILIONI 33.7 ZIMETUMIKA KUTEKELEZA ELIMU YA MSINGI BILA MALIPO MKOANI IRINGA (ILANI YA CCM 2015-2020)

Image
  ILANI YA CCM (2015-2020) MKOA WA IRINGA Jumla ya Sh 33.7 Bilioni zimetumika kugharamia Elimu ya Msingi Bila Malipo katika kipindi cha mwaka 2015-2020. Tumetekeleza kwa Kish indo, Tunasonga Mbele Pamoja

HAWA NDIO WASANII WATAKAO PAMBA UWANJA WA SAMORA JUMATATU, HII SIO YA KUKOSA!

Image
                                                             Hii ndiyo orodha ya wasanii watakaopamba uwanja wa Samora siku ya Jumatatu, Septemba 28,2020. Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Rais Dk John Pombe Magufuli atahutubia mamia ya wakazi wa Iringa. 1.Shilole 2.Aslay 3.Becka 4.Enock 5.Mr Blue 6.Rayvanny 7.Bwax 8.Harmonize 9.Maua 10. Ezenice 11. Nyamidela Na wengine wengi kutoka ndani na nje ya Iringa  

TAARIFA YA UJIO WA MGOMBEA URAIS WA CCM, DK JOHN MAGUFULI KUTOKA OFISI ZA CCM MKOA WA IRINGA

Image
 CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA IRINGA NDUGU WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI PAMOJA NA WANANCHI WOTE WA IRINGA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA IRINGA KINAWAKARIBISHA KATIKA MKUTANO WAKE WA HADHARA UTAKAOFANYIKA KATIKA UWANJA WA SAMORA MKUTANO HUO UTAHUDHURIWA NA MH RAIS DR JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI AMBAYE PIA NI MGOMBEA URAIS KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI KUPITIA MKUTANO HUO MH RAIS DR JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI ATAELEZEA KWA KINA NAMNA ILANI YA 2015/2020 ILIVYOTEKELEZWA KWA MAFANIKIO PIA ATAELEZEA KWA KINA YALIYOMO KATIKA ILANI YA UCHAGUZI YA 2020-2025 HII SI YAKUKOSA, KARIBU SANA UWANJA WA SAMORA TAREHE 28/09/2020 TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA # MAGUFULI5TENA # HAPAKAZITU # CCM✓ # WABUNGE✓ # MADIWANI✓

JIMBONI ISIMANI KUNAZIDI KUNOGA - WANANCHI WAMUAHIDI LUKUVI KURA ZA KISHINDO

Image
  Wananchi wa Jimbo la Isimani, Iringa vijijini wameahidi kumchagua Mh William Lukuvi kwa kumpa kura za kutosha kutokana na kazi kubwa aliyoifanya jimboni humo katika kuwaletea maendeleo. Pia, wameahidi kura za kutosha kwa Rais John Pombe Magufuli na madiwani wote. Katika mkutano uliofanyika katika kata ya Malengamakali kwenye  Vijiji vya Nyakavangala, Mkulula na Usolanga, Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa Theresia Mtewele alitumia nafasi hiyo kuomba kura akisisitiza wananchi wajitokeze kwa wingi siku hiyo. Mwenyekiti wa UVCCM wilaya Iringa Vijijini Ndg Makala Mapesah Johnson Juma aliwaambia  wananchi wote kuwa Mwaka huu Kata ya Malengamakali tumepata watu hodari kuanzia kwenye kata MH Stephano Mkisi kama Diwani wetu na

Dk Kabati aongoza kusaka kura za Rais kwa wanawake wanaofanya kazi Bar

Image
Mbunge mteule wa Viti Maalum mkoa wa Iringa (CCM), Dk Ritta Kabati kwa kushirikiana na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM Iringa Mjini ameongoza harakati za kutafuta kura za Rais, wabunge na madiwani kwa wanawake wanaofanya kazi Bar. Dk Kabati amewataka wanawake hao kuipigia kura CCM kwa sababu yapo mambo mengi yaliyofanyika chini ya utawala wa awamu ya tano unaoongozwa na Rais John Pombe Magufuli. Aidha, Kabati amewaomba wanawake hao kumchagua, Dkt. Jesca Msambatavangu kuwa Mbunge wa Iringa mjini ili asaidie katika kuleta maendeleo.

UVCCM MKOA WA IRINGA KUONGOZA MATEMBEZI YA KUMPOKEA MGOMBEA URAIS WA CCM

Image
Umoja wa Vijana Mkoa wa Iringa unawakaribisha wananchi wote wa Mkoa wa Iringa kwenye matembezi ya kumpokea Mgombea Urais wa CCM, Rais John Pombe Magufuli Jumapili Tarehe 27/2020. Matembezi yataanza saa 2.00 asubuhi Stendi ya zamani.

SAMORA KUMEKUCHAAAA!

Image
  "karibuni sana siku ya Jumatatu kumsikiliza Rais John Pombe Magufuli katika mkutano mkubwa utakaofanyika katika uwanja wa Samora, Mjini Iringa kuanzia saa 12 asubuhi"-Brown Mwangomale-Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa

CHUMI ANATOSHA JIMBO LA MAFINGA MJINI

Image
  Wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini wamesema, CCM haikukosea kumteua Mh Cosato Chumi kuwania Ubunge Jimbo la Mafinga Mjini. Chumi anaendelea kuomba kura za ndio kwa nafasi yake ya Ubunge, madiwani na kura za kujaa na kumwagika kwa Rais John Pombe Magufuli.

"Isimani tuna Mbunge Jembe " - Amosi Makala

Image
   Mwenyekiti wa UVCCM - Iringa Vijijini amesema Jimbo la Isimani linayo bahati kumpata mbunge jembe, Mh Willium Lukuvi ambaye anatambua changamoto za wananchi wake na mikakati ya namna ya kutatua. "Tuna Mbunge Jembe lisiloisha makali"

IRINGA MJINI NI JESCCA MSAMBATAVANGU

Image
Mgombea Ubunge kupitia CCM, Jesca Msambatavangu ameendelea kuchanja mbuga za kuomba ridhaa ya kuongoza jimbo hilo. Jesca Msambatavangu ndiye habari ya Iringa Mjini....

"CCM tunafanya kampeni za kistaarabu"- Mh Polepole

Image
  Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mh Humphrey Polepole amesema chama hicho kimekuwa kikiendesha kampeni za kistaarabu zilizojikita katika kutoa hoja, sababu, kueleza sera pamoja na  yote ambayo yanaonyesha CCM imetoka wapi na inaelekea wapi. Pia Mh Polepole amempongeza mgombea wa CCM, Rais John Pombe Magufuli kuwa mstari wa mbele katika kuendesha kampeni hizo za kistaarabu. Kiongozi huyo wa CCM amezungumza hayo leo Septemba 25, 2020 wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma. "Tunampongeza Rais Magufuli katika hilo" anasema Polepole na kluongeza; "Bahati mbaya sana wapinzani wamekuwa mstari wa mbele kutumia uongo kama nyenzo ya kampeni! uongo mkubwa, upotoshaji wa makusudi, mi nimesjindwa kuelewa lakini uzuri watanzania wanajua uongo,"

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020

Image
Mgombea wa CCM, Rais Dkt John Pombe Magufuli anatarajia kuhutumia maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Iringa, siku ya Jumatatu, Septemba 2020. Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Brown Mwangomale amesema atahutumia mamia ya wakazi wa Mkoa wa Iringa katika uwanja wa Samora, mjini Iringa. Amewakaribisha wanananchi na wanaccm wote kujitokeza kwa wingi ili kumlaki Rais Magufuli.