CHUMI AFUNGA KAMPENI KWA KUAINISHA VIPAUMBELE, HANA MPINZANI MAFINGA MJINI


Chumi afunga kampeni Mafinga Mjini kwa kuweka bayana vipaumbele vyake

 Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, Cosato Chumi amefunga kampeni huku akiweka wazi vipaumbele vyake.

 

1. Miundombinu ya barabara

Ni kuhakikisha kuwa tunajenga kilomita kadhaa za lami na Taa za Barabarani ndani ya Mji wa Mafinga.

 

2. Afya, 

Kukamilisha Miradi ya ujenzi wa Kituo Cha Afya Bumilayinga, kuanza ujenzi wa Kituo Cha Afya Kata ya Upendo   na kukamilisha taratibu za kupata vibali na vifaa Tiba ili majengo yaliyokuwa yakitumiwa na Mkandarasi wa barabara ya Mafinga Igawa ambayo tulimuomba Mhe Rais Magufuli alipofanya ziara hapa Mafinga yaanze kutumika kama Kituo cha Afya cha Changarawe.

2. Elimu,

a) Elimu ya Msingi, kuhakikisha kuwa tunajenga shule ya Msingi maeneo ya Ndolezi-(Kata ya Boma), Lumwago (Kata ya Upendo) na Iditima (Kata ya Bumilayinga)

 

b) Elimu ya Sekondari -Kuhakikisha tunakamilisha ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Sao Hill na kuongeza majengo ya Maabara Shule ya Sekondari ya Upendo

- kuhakikisha tunajenga Hostels/mabweni Ili kuwapunguzia watoto taabu ya kutembea umbali mrefu kutoka na kwenda shuleni.

 

4. Umeme Pamoja na kuwa tumefikisha Umeme kila kijiji na baadhi ya mitaa, bado haujafika kila Kitongoji, hivyo jukumu la sasa ni kuhakikisha kuwa maeneo na vitongoji vyote ambavyo havijafikiwa umeme unafika ili kuchochea shughuli za uzalishaji Mali na Kujiongezea kipato.

 

5. Maji,  tunatarajia kutokana na fedha za mkopo wa riba nafuu kutoka India dola 500m Sawa na zaidi ya trilioni 1.2, maarufu kama Mradi wa Miji 28, sisi ni sehemu ya wanufaika wa fedha Hizi, tunamaliza kero ya maji katika maeneo yote ya Mji wa Mafinga.

 

6. Uchumi, ujasiriamali na biashara

Pamoja na kuongeza ufanisi katika mikopo ya Vijana, Wanawake na watu wenye ulemavu, tutahakikisha kuwa maeneo yaliyochangamka kibiashara yanaruhusiwa kufanya biashara masaa ishirini na manne, sambamba na Kuboresha mafunzo ya ujasiriamali na Kuboresha mazingira ya kufanyia biashara zote muhimu ikiwemo biashara ya mazao ya misitu.

 

Ndio maana tunasema kazi ni Moja tu tarehe 28 Oktoba Ku-connect Diwani wa CCM, Mbunge Chumi afu Tunamalizia JPM-Magufuli






Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020