JESCA AFUNGA KAMPENI KWA KISHINDO IRINGA MJINI, UWANJA WANONA

 

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini (CCM) Jesca Msambatavangu jana amefunga kampeni zake kwa kishindo baada ya umati mkubwa wa watu kufika katika uwanja wa Mwembetogwa ili kusikiliza sera zake.

Mnec na Mbunge wa Jimbo la Mtera, David Lusinde alimnadi Jesca Msambatavangu akiwataka wana Iringa kumchagua ili awawakilishe Bungeni.

Mnec wa Mkoa wa Iringa, Salim Asas aliwataka wakazi wa Mkoa wa Iringa wasifanye kosa na badala yake wahakikishe wanakipigia Chama cha Mapinduzi kwa nafasi zote.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Said Rubeya aliwashukuru wananchi wa Iringa kwa ushirikiano wao wakati wa kampeni na kuwaomba wasisahau CCM hapo kesho, siku ya uchaguzi.













Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020