HILARY KIPINGI AKONGA NYOYO ZA MABALOZI WA NYUMBA KUMI MASHABIKI WA YANGA ulipuka kwa shangwe!

 

Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Hilary Kipingi amesababisha makofi na vifijo huku akiacha mashabiki wa Simba wakitulia baada ya kutoa pongezi za ushindi wa Yanga katika mtanange uliochezwa huko Zanzibar.

 

Kipingi alitoa pongezi za ushindi wa Yanga kwenye mkutano uliowakutanisha mabalozi wa CCM na Mlezi wa CCM mkoa wa Iringa, Mh Mizengo Pinda.

 

“Hongera sana wana Yanga kwa ushindi mnono wa Jana, na Simba vumilieni tu. Yanga hoyeeee!” alisema Kipingi.

 

Kuhusu CCM, Kipingi amesema mabalozi ni kati ya makundi hayo, na kwamba kundi hilo limechangia ushindi mkubwa wa CCM.

 

“Mabalozi wamefanya kazi kubwa sana, tunawapongeza sana na tunawashukuru kwa hilo,” amesema.





Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020