Ibrahim Ngwada; Msiruhusu wageni kulala na watoto majumbani kwenu

 

Meya wa Manispaa ya Iringa, Ibrahim Ngwada ameitaka jamii ya wakazi wa Manispaa ya Iringa kuwalinda watoto na kutoruhusu wageni wasilale nao wakati wanapowatembelea nyumbani kwao

Amesema matukio mengi ya ukatili kwa watoto hufanywa na watu wa karibu ambao huwa wanaaminiwa na kuachwa wawe karibu na watoto hata kwenye mazingira hatarishi.

"Tusipowalinda watoto hatutapata taifa bora lenye viongozi imara, tuwalinde tangu huko nyumbani, tusiwaach walale na watoto" amesema Mh Ngwada.


Ngwada amezungumzia jambo hilo kutokana na mkakati wake wa kuhakikisha watoto wanalindwa, kutunzwa na kuheshimiwa.

Mh Ngwada alizungumza hayo jana wakati wa maandalizi ya video ya wimbo wa *MTOTO WA AFRIKA* ya Dkt Tumaini Msowoya unaosimamiwa kwa pamoja kati ya unaofanywa chini ya kampuni ya Home Studio Production ya Arusha na SCALLET Video Production ya Jijini Dar es Salaam.

 


Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020