Kikao cha Mabalozi wa CCM Iringa Mjini chaibua kero ya bili kubwa ya maji.


Kikao cha Mabalozi wa CCM kimeibua kero ya bili kubwa za maji, jambo lililosababisha viongozi, akiwemo Waziri Mkuu na Mlezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Mizengo Pinda kuzungumzia.

Hoja hiyo iliibuliwa na wananchi, hivyo Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini, Richard Kasesela, Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu kuahidi kukutana na Waziri wa Maji, ili kutatua kero hiyo.

Awali, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Dr Abel Nyamahanga, Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Brown Mwangomale na Mwenyekiti wa CCM wa Iringa Mjini, Said Rubeya walisema, maji imekuwa kero ambayo inapaswa kushughulikiwa.

“Utadhani tunaagiza maji China? Bili ya maji Iringa ni kubwa sana” amesema Myamahanga.

Mbunge Jesca Msambatavangu alisema jambo hilo wameanza kulishughulikia na kwamba, kazi iliyobaki ni kwenda kwa waziri wa maji kuona walau, maji yanayotoka Iringa mjini yawe na ruzuku ili kupunguza mzigo kwa wananchi.

Hoja ya kumuona waziri, ilizungumzwa pia na Mh Kasesela  aliyesema kero hiyo imemfikia hivyo inapaswa kuchukuliwa hatua zaidi.



 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020