MNEC wa Iringa, Salim Asas awavunja mbavu wabunge na madiwani, Asema Paka waliyemchagua 2017 amekamata Panya wote Iringa.

 Huku akiwavunja mbavu wabunge na Madiwani wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa wa Iringa, Salim Abri Asas amekumbushia maneno aliyotumia mwaka 2017 wakati akiomba nafasi hiyo ya kuwaomba wajumbe, wasichague aina ya paka wanayetaka akamate panya.

Mnec alikuwa akizungumza na wabunge na wajumbe katika Mkutano Maalum wa Wabunge na Madiwani uliokuwa unaongozwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda ambaye pia ni Mlezi wa CCM wa Mkoa wa Iringa.


Salim amesema aliwaambia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wa Mkoa wa Iringa kwamba, ili ushindi upatikane katika jimbo la Iringa na kata zenye upinzani, wasiangalie rangi ya paka atakayekamata panya.

“Niliema nitahakikisha CCM inapata ushindi wa kishindo 2020, niliwaambia ukiwa na panya hushauriwi kuchagua rangi ya Paka. Kuna panya wanatusumbua jamani?” alihoji Salim Asas.





Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa akimkaribisha Salim Asas, Mnec wa Iringa kuzungumza na wabunge na madiwani.






Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020