UTEKELEZAJI WA ILANI; IDARA YA ELIMU MKOA WA IRINGA YAWAFIKIA WATOTO WENYE ULEMAVU


Afisa Elimu wa Mkoa wa Iringa, Germana Mung'aho amesema wanaendelea kutekeleza Ilani ya CCM kwa kuhakikisha kila mtoto anapata haki ya msingi ya kupata elimu, kwa kuwafikia watoto wenye ulemavu.

Amesema tayari wameendesha zoezi la ubainishaji wa watoto hao, na wanaandaliwa fursa ya kupata elimu kulingana na aina ya ulemavu wao.

"Kuna watoto watapelekwa kwenye elimu jumuishi na wengine elimu maalum kulingana na ulemavu wao. Sera ya watu wenye ulemavu na Ilani ya CCM vyote vinataja haki sawa kwa watoto bila ubaguzi," amesema.



Ofisa Elimu ya watu Maalum, Iringa Vijijini Vumilia Chaki, amesema hiyo ni fursa kwa watoto wenye ulemavu kupata haki zao.

"Kuna watoto ambao hawapati haki zao kwa sababu tu wapo mbali na maeneo ya shule au, kwa kuwa familia zao zina kipato duni,"amesema.

Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

MKAKATI MKAKATINI AWAMU YA PILI KUTIKISA IRINGA

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

RAIS MAGUFULI KUTUA IRINGA JUMATATU, SEPTEMBA 28, 2020