MIAKA 44 YA KUZALIWA KWA CCM - UWT MKOA WA IRINGA YAANDAA MAKUBWA

Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Iringa umeandaa shughuli kabambe katika kuadhimisha miaka 44 ya kuzaliwa kwa CCM ikiwamo kupima magonjwa mbalimbali bure na uchangiaji wa damu. Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Iringa, Nikolina Luandala na Katibu wa UWT Mkoa wa Iringa, Angela Milembe wamesema maadhimisho hayo yatafanyika katika uwanja wa Mwembetogwa, February 1, 2021 kuanzia saa mbili kamili asubuhi . Magonjwa mengine yatakayopimwa ni magonjwa ya moyo, Kisukari, saratani ya matiti na saratari ya uzazi. Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (MNEC) Salim Asas