Posts

KAMATI YA SIASA YA CCM YAENDELEA NA ZIARA KUKAGUA MIRADI YA MAJI VIJIJINI

Image
  Kamati ya Siasa ya CCM ikiongozwa na Mwenyekiti Dr Abel Nyamahanga, inaendelea lea na ziara ya kukagua miradi ya maji Vijijini nayosimamiwa na Wakala wa Maji Safi na Mazingira Vijijini (RUWASA) Lengo okubwa la ziara hiyo ni kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya kuhakikisha wananchi vijijini wanpatiwa maji safi na salama ili kumtua mama ndoo kichwani.

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AMALIZA ZIARA MKOA WA IRINGA KWA KUTEMBELEA IRINGA MJINI

Image
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi na Mjumbe wa kamati kuu ya CCM taifa Komred Kheri James leo amehitimisha ziara ya kikazi Mkoani iringa katika wilaya ya iringa mjini. Katika Ziara hiyo ya kukagua na kuimarisha Uhai wa Chama na Jumuiya pamoja na kuzungumza na mabaraza yote ya Jumuiya za CCM imekamilika kwa Mwenyekiti  kutembelea Wilaya zote za Mkoa wa Iringa ikiwemo Mufindi,Kilolo,iringa Vijijini na Iringa Mjini. Akizungumza na wajumbe wa Halimashauri kuu ya CCM Wilaya pamoja na Wanachama Komred kheri James  ametoa pongezi kwa Viongozi na  wanachama wa CCM wa wilaya ya Iringa Mjini kwa Ushindi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 kwa kurejesha jimbo La Iringa Mjini kwa Chama Cha Mapinduzi na Ushindi wa Kata zote. Pia komred kheri James awasihi Viongozi wa Chama na Serikali kuendeleza Umoja na Mshikamano kwa kuhudumia na kutatua  Kero mbalimbali za wananchi na kuwataka Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kuendelea kutimiza wajibu wa Kuisimamia na K...

SIKU YA TATU YA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA COMRADE KHERI JAMES; ATEMBELEA IRINGA VIJIJINI

Image
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi na Mjumbe wa kamati kuu ya CCM taifa Komred Kheri James leo ameendelea na Ziara yake ya kikazi ya kuimarisha Uhai wa Chama na Jumuiya katika wilaya ya Iringa Vijijini Mkoa Iringa. Akiwa wilayani humo komred Kheri James amezungumza na Mabaraza yote ya Jumuiya za CCM wilayani humo Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Siasa Na kilimo. Akizungumza na wajumbe wa Mabaraza hayo Komred kheri James amewasihi kuendelea kisimamia Serikali katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ili kuleta maendeleo na ustawi wa wananchi kama tulivyowaahidi katika uchaguzi Mkuu uliopita. Aidha Komred Kheri James ametoa pongezi za dhati kwa Halimashauri ya iringa Vijijini kwa kutekeleza kwa vitendo zoezi la uwezesheji wa vijana kiuchumi jambo ambalo limechochea vijana kuwa wabunifu na kujiajiri katika shughuli mbali mbali za uzalishaji mali. Akikamilisha ziara yake wilayani iringa Vijijini komred kheri James allipata fursa ya kutembelea Shamba la Umoja wa Vijana...

SIKU YA PILI YA ZIARA; MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA, KHERI JAMES ATEMBELEA KILOLO

Image
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi komred kheri D James leo ameendelea na Ziara ya kikazi ya kuimarisha Uhai wa Chama na Jumuia mkoa wa Iringa katika Wilaya ya kilolo. Akiwa wilayani Kilolo, Komred Kheri James amehimiza umuhimu wa jamii kuendelea kuwalea,kuwainua,kuwajengea uwezo na kuwapa fursa vijana ktk shughuli na majukumu mbalimbali ya kijamii,kiuchumi na kisiasa Ili kuwaandaa kuwa raia bora na viongozi imara na wenye tija kwa Taifa.            "Jukumu la kuwalea,kuwajengea uwezo,na kuwaandaa vijana kwa maslahi ya leo na kesho ya Nchi yetu sio jambo la hiyari,ni wajibu wa lazima kwa jamii yote kwa faida ya leo na kesho ya Taifa letu" Alisema  Komred Kheri James Pia Komred kheri James  amepongeza kamati ya siasa ya Wilaya ya Kilolo ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo kwa kuanza ujenzi wa Ofisi ya CCM ya kisasa katika wilaya hiyo. Aidha komred kheri James amewatak...

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI; BI ANGELA MILEMBE - KATIBU WA UWT MKOA WA IRINGA

Image
                               *KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI*                                                                     BI ANJELA MILEMBE                                                         KATIBU WA UWT MKOA WA IRINGA             "Tufanye kazi kwa bidii, tuendelee kuwa waadilifu na tuhakikishe tunarithisha vizazi vyetu tabia njema ili kuandaa kizazi kijacho. Mwanamke akiaminiwa na kupewa nafasi anaweza kufanya maajabu" HERI YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MACHI 8,2021

HERI JAMES; MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AANZA ZIARA MKOANI IRINGA

Image
  Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Comrade Hery James ameanza ziara ya kikazi Mkoani Iringa ikiwa na lengo la kuimarisha Jumuiya ya Umoja wa Vijana. Katika ziara yake, Comrade Heri ametembelea wilaya ya Mufindi na kukutana na mabaraza ya Jumuiya za UWT, WAZAZI NA VIJANA. Katika ziara hiyo, kiongozi huyo wa Jumuiya ya Vijana alisisitiza upendo, umoja na mshikamano kama njia pekee ya kuendelea kukijenga chama cha mapinduzi. Amesema uchaguzi wa mwaka jana CCM ilifanikiwa kwa sababu ya ukwelina kuwataka vijana wasomi, watumie elimu yao kwa manufaa ya jamii na chama.

KATIBU WA CCM IRINGA, MWANGOMALE AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI, KUIMARISHA UHAI WA CHAMA

Image
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Ndugu Brown Mwangomale amefanya ziara ya kuimarisha uhai wa chama hicho wilayani Mufindi kwa lengo la kukagua ujenzi nyumba ya katibu wa CCM wilaya ya Mufindi. Katika ziara hiyo, Mwangomale ambaye aliongozana na Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Sadick Kadulo ameagiza ujenzi wa nyumba hiyo uanze mara moja baada ya kusimama kwa miaka mingi, bila kuendelezwa. Pia, Mwangomale ametembelea viwanja viwili vya CCM vilivyopo karibu na kituo cha Polisi na kuishauri CCM Wilaya ya Mufindi kujenga hoteli ya kisasa, itakayosaidia kuongeza mapato. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Katibu wa CCM Wilaya ya Mufindi, James Mgego ameahidi kutekeleza maagizo ya Mwangomale na kwamba ameahidi kusimamia ujenzi wa nyumba hiyo sambamba na uendelezaji wa viwanja vya CCM. Kuhusu uwanja wa Mpira, Mwangomale ameiomba CCM Makao Makuu kusaidia ujenzi wa kisasa kwenye uwanja huo ili kuendeleza sekta ya michezo ndani ya mkoa wa Iringa.

UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM- MKOA WA IRINGA WAENDELEZA MIKAKATI KUTOKOMEZA NA UTAPIAMLO HASA KWA WATOTO

Image
  Afisa Lishe wa Mkoa wa Iringa, Neema Mtekwa amesema wanaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali katika kukabiliana na utapiamlo kwa watoto mkoani Iringa. Mikakati hiyo inatekelezwa wakati ambapo asilimia 47 ya watoto mkoani humo wanaudumavu, asilimia 3.7 wana ukondefu na asilimia sita wana ukondefu. Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 inasisitisha lishe bora kwa watoto na kupambana na tatizo la utapiamlo. Miongoni mwa mikakati hiyo ni elimu kwa jamii juu ya ulaji mlo kamili, matibabu sahihi kwa wale waliopata ugonjwa huo, utoaji wa virutubisho nyongeza na unyaji wa maziwa shuleni. Mikakati mingine ni kuhamaisha wazee wa kimila, viongozi wa dini kuzungumzia suala la lishe, kulifanya suala la lishe kama agenda kwenye vikao sambamba na kuwa na clubs za wanafunzi ili wajadili jambo hilo.  

UTEKELEZAJI WA ILANI; IDARA YA ELIMU MKOA WA IRINGA YAWAFIKIA WATOTO WENYE ULEMAVU

Image
Afisa Elimu wa Mkoa wa Iringa, Germana Mung'aho amesema wanaendelea kutekeleza Ilani ya CCM kwa kuhakikisha kila mtoto anapata haki ya msingi ya kupata elimu, kwa kuwafikia watoto wenye ulemavu. Amesema tayari wameendesha zoezi la ubainishaji wa watoto hao, na wanaandaliwa fursa ya kupata elimu kulingana na aina ya ulemavu wao. "Kuna watoto watapelekwa kwenye elimu jumuishi na wengine elimu maalum kulingana na ulemavu wao. Sera ya watu wenye ulemavu na Ilani ya CCM vyote vinataja haki sawa kwa watoto bila ubaguzi," amesema. Ofisa Elimu ya watu Maalum, Iringa Vijijini Vumilia Chaki, amesema hiyo ni fursa kwa watoto wenye ulemavu kupata haki zao. "Kuna watoto ambao hawapati haki zao kwa sababu tu wapo mbali na maeneo ya shule au, kwa kuwa familia zao zina kipato duni,"amesema.

MIAKA 44 YA KUZALIWA KWA CCM - UWT MKOA WA IRINGA YAANDAA MAKUBWA

Image
Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Iringa umeandaa shughuli kabambe katika kuadhimisha miaka 44 ya kuzaliwa kwa CCM ikiwamo kupima magonjwa mbalimbali bure na uchangiaji wa damu. Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Iringa, Nikolina Luandala na Katibu wa UWT Mkoa wa Iringa, Angela Milembe wamesema maadhimisho hayo yatafanyika katika uwanja wa Mwembetogwa, February 1, 2021 kuanzia saa mbili kamili asubuhi . Magonjwa mengine yatakayopimwa ni magonjwa ya moyo,  Kisukari, saratani ya matiti na saratari ya uzazi. Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (MNEC) Salim Asas

KATIBU WA UVCCM TAIFA MWALIMU MWANGWALA AKUTANA NA VIJANA WA UVCCM IRINGA MJINI

Image
  kATIBU Mkuu wa UVCCM Taifa, Mwalimu RAYMOND MWANGWALA amekutana na kufanya mazungumzo na vijana wa UVCCM Iringa mjini. Mwangwala amewashukuru vijana hao kwa jitihada zao za kusaidia ushindi wa Jimbo la Iringa Mjini. Katika kikao hicho, Mwenyekiti wake Ndg Salvatory Ngerera pia aliwashukuru  vijana kwa kazi kubwa walioifanya katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 ambapo matokeo yake ni ushindi wa kishindo wa CCM Iringa Mjini. Katika kikao hicho pia Umoja wa Vijana umewashukuru na kuwapa hati za pongezi viongozi na makada wote ambao wakati wote wamekuwa walezi wa vijana katika wilaya hiyo wakiongozwa na MNEC wa CCM Mkoa wa IRINGA Ndg Salim F Abri

Ibrahim Ngwada; Msiruhusu wageni kulala na watoto majumbani kwenu

Image
  Meya wa Manispaa ya Iringa, Ibrahim Ngwada ameitaka jamii ya wakazi wa Manispaa ya Iringa kuwalinda watoto na kutoruhusu wageni wasilale nao wakati wanapowatembelea nyumbani kwao Amesema matukio mengi ya ukatili kwa watoto hufanywa na watu wa karibu ambao huwa wanaaminiwa na kuachwa wawe karibu na watoto hata kwenye mazingira hatarishi. "Tusipowalinda watoto hatutapata taifa bora lenye viongozi imara, tuwalinde tangu huko nyumbani, tusiwaach walale na watoto" amesema Mh Ngwada. Ngwada amezungumzia jambo hilo kutokana na mkakati wake wa kuhakikisha watoto wanalindwa, kutunzwa na kuheshimiwa. Mh Ngwada alizungumza hayo jana wakati wa maandalizi ya video ya wimbo wa *MTOTO WA AFRIKA* ya Dkt Tumaini Msowoya unaosimamiwa kwa pamoja kati ya unaofanywa chini ya kampuni ya Home Studio Production ya Arusha na SCALLET Video Production ya Jijini Dar es Salaam.  

Uhai wa CCM; Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa akikagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi ya CCM Kilolo na nyumba ya UVCCM

Image
  Ukizungumzia uhai wa chama ni pamoja na uwepo wa ofisi nzuri na nyumba za watendaji. Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Brown Mwangomale na viongozi wengine wa CCM Mkoa wa Iringa, wamefanya ziara kukagua nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Iringa na Ofisi ya CCM Wilaya ya Kilolo.  

HILARY KIPINGI AKONGA NYOYO ZA MABALOZI WA NYUMBA KUMI MASHABIKI WA YANGA ulipuka kwa shangwe!

Image
  Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Hilary Kipingi amesababisha makofi na vifijo huku akiacha mashabiki wa Simba wakitulia baada ya kutoa pongezi za ushindi wa Yanga katika mtanange uliochezwa huko Zanzibar.   Kipingi alitoa pongezi za ushindi wa Yanga kwenye mkutano uliowakutanisha mabalozi wa CCM na Mlezi wa CCM mkoa wa Iringa, Mh Mizengo Pinda.   “Hongera sana wana Yanga kwa ushindi mnono wa Jana, na Simba vumilieni tu. Yanga hoyeeee!” alisema Kipingi.   Kuhusu CCM, Kipingi amesema mabalozi ni kati ya makundi hayo, na kwamba kundi hilo limechangia ushindi mkubwa wa CCM.   “Mabalozi wamefanya kazi kubwa sana, tunawapongeza sana na tunawashukuru kwa hilo,” amesema.

JESCA MSAMBATAVANGU; *TUMEIBUKA TUKIWA NA NGUVU*

Image
  Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu amesema licha ya miaka kumi jimbo hilo kuwa upinzani, CCM imeibuka tena ikiwa na nguvu.   Jesca alikuwa akiwashukuru mabalozi wa nyumba kumi katika kikao kilichokuwa kinaongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.   Amewashukuru mabalozi wa nyumba kumi kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kuhakikisha kuwa wanasimamia ushindi wa kishondo kwa Rais Magufuli, wabunge na madiwani.   “Mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa walikuwa wanapata shuda kukusanya kero za wananchi lakini sasa tupo, tutafanya kazi hiyo kuwapunguzia mzigo,” amesema Msambatavangu.        

DC Kasesela; Wananchi endeleeni kuijengea imani na Serikali yenu

Image
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela amesema wananchi wanapaswa kuendelea kujenga Imani kwa Serikali yao kwa sababu inaendelea kusikiliza na kutatua kero zao. Amesema kati ya kero zilizomfikia mezani kwake kutoka manispaa ya Iringa ni bili kubwa za maji na ukatili wa kijinsia. DC Kasesela alikuwa akizungumza leo katika kikao cha mabalozi wa nyumba kumi kilichokuwa kikiongozwa na Wairi Mkuu Mtaafu, Mh Pinda. “Kuna kero nyingine wanawake wanapigwa na waume zao, na wanaume nao wanapigwa na wake zao, haya yote tunashughulikia,” amesema DC Ksesela. Aidha amewapongeza mabalozi wa CCM kwa kuipambania CCM na kusababisha ushindi wa kishindo manispaa ya Iringa.

IBRAHIM NGWADA; TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMISI YA MWISHO WA MWEZI

Image
  Meya wa Manispaa ya Iringa, Ibrahim Ngwada ameamua kutenga siku moja kila mwezi ka ajili ya kusikiliza kero za wananchi, kuhusu migogoro ya ardhi. Amesema kila Alhamisi ya mwisho wa mwezi itakuwa muafaka kwake akishirikiana na wataalamu wa ardhi kuketi na kuwasikiliza wananchi wa Manispaa ya Iringa. Ngwada alikuwa akizungumza leo katika kikao cha mabalozi wa nyumba kumi ambacho Waziri Mkuu Mstaafu na Mezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Mizengo Pinda. Amesema migogoro ya ardhi ni kati ya kero alizokutana tangu aapishwe kuwa Meya wa Manispaa ya Iringa. Kero nyingine za wananchi alizoahidi kupambana nazo ni tabia ya baadhi wa watendaji wa mitaa na kata kutaka rushwa wanapotakiwa kutoa barua za dhamana. Mh Ngwada amesema wamepania kubuni vyanzo vingi vya mapato ili kukuza uchumi wa manispaa na kuondoa tozo ndogo dogo zinazowamiza wananchi. “Tumekubaliana kushirikiana kwa kiasi kikubwa mimi na Mbunge, Mh Jesca Msambatavangu na tumejipanga kuhakikisha kunakuwa na mabadiliko,” amesema.

POKEENI SIMU ZA WANANCHI - DR NYAMAHANGA

Image
  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Dk Abel Nyamahanga amewataka viongozi waliochaguliwa kwa kupigiwa kura kujenga tabia ya kupokea simu za wananchi. Nyamahanga alikuwa akizungumza kwenye kikao cha mabalozi wa nyumba kumi waliokutana kwa ajili ya kupewa shukrani toka kwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mlezi wa CCM Iringa, Mizengo Pinda. Amesema hakuna mkubwa zaidi ya wananchi waliowapa dhamana ya kuwa viongozi kwenye maeneo yao. “Pokeeni simu, hakuna mkubwa kwenye chama hiki , wakubwa ni wananchi waliowachagua nyie. Fanyeni kazi na pokeeni simu,” amesema. Amesema ipo tabia ya baadhi ya viongozi wa kata kujifanya miungu watu wa kuwachaji fedha wananchi wanaoenda kuomba dhamana